Uhuru Publications Ltd - Gazeti Uhuru, Mzalendo na Burudani

Friday
Jul 30th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home Habari za Kitaifa Personal Tech Mtoto azinduka kabla ya maziko

Mtoto azinduka kabla ya maziko

E-mail Print PDF

NA KHADIJA MUSSA

BAADHI ya madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Hindu Mandal, Dar es Salaam, wanadaiwa kutoa taarifa za uongo kwamba mtoto aliyezaliwa amekufa, lakini muda mfupi baadae alibainika kuwa yu hai. Tukio hilo lililoacha maswali mengi lilitotokea juzi saa moja usiku, ambapo uongozi wa hospitali hiyo ulithibitisha kutokea, huku ukitia shaka juu ya mazingira yake. Habari zilizopatikana hospitalini hapo zilidai mjamzito aliyejifungua mtoto huyo alifikishwa hospitalini hapo kichanga hicho cha kiume kikiwa kimeanza kutoka. Ilidaiwa baada ya mjamzito huyo kusaidiwa na kumaliza kujifungua, alielezwa mwanawe amekufa, hivyo walikabidhiwa kichanga hicho kwa ajili ya maziko. Kwa mujibu wa chanzo cha habari, baada ya kufika nyumbani wakijiandaa na mazishi ya mtoto huyo, baba yake alipewa taarifa za kifo na aliomba asizikwe hadi atakapofika. Ilidaiwa baada ya baba huyo kufika nyumbani, mtoto huyo aliyekuwa amefunikwa nguo alipofunuliwa alionyesha dalili za kuwa hai, huku akijinyoosha, jambo lililowafanya wamrudishe hospitalini hapo. Chanzo hicho kilidai baada ya kufikishwa hospitalini, kichanga hicho kiliwekwa kwenye kifaa maalumu kinachotumika zaidi kwa watoto njiti. Imeelezwa kuwa kichanga hicho kilikaa katika kifaa hicho kwa saa tano, kabla daktari kueleza kuwa kimekufa. Habari zaidi zilidai baada ya uongozi wa hospitali kupata taarifa za kifo hicho, ulimrudishia mama mzazi sh. 400,000, fedha alizotoa kwa ajili ya huduma za kujifungua. Akizungumzia suala hilo jana, Dk. Kaushik Ramaiya, alisema walipata taarifa za tukio hilo juzi kutoka kwa daktari aliyekuwa zamu. Dk. Kaushik alisema mama huyo alifika hospitalini hapo akitokea hospitali ya Dar Group, akiwa katika hatua za mwisho za kujifungua. Alisema mama huyo alihudumiwa na daktari aliyemtaja kwa jina moja la Dk. Charles. "Baada ya mtoto kuzaliwa alionekana hana dalili za kuwa hai, wauguzi walitumia njia zote na  walipothibitisha amefariki waliamua kumweleza mzazi kuwa mtoto amekufa. "Nilishangaa kusikia baba na shangazi wa mtoto huyo walisema walipofika nyumbani waliona mtoto anaanza kupumua na kumrudisha ambapo wauguzi walikiri anapumua na kumweka katika mashine,” alisema Dk. Kaushik. Hata hivyo, alisema tukio hilo ni la  ajabu kwani halijawahi kutokea tangu aanze kazi ya udaktari miaka 29 iliyopita. Alisema wauguzi na daktari aliyekuwa zamu wakati wa tukio wametakiwa kutoa maelezo na kwamba uchunguzi unaendelea. Kuhusu mzazi kurudishiwa fedha, Dk. Kaushik alisema walifanya hivyo kwa ajili ya ubinadamu na si kwa nia nyingine yoyote.

Last Updated ( Thursday, 11 March 2010 09:40 )  

Kutoka Magazetini

 

RAIS wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, ametoa mwaliko kwa timu ya taifa ya Ghana

 

MKURUGENZI wa (TFF) Sunday Kayuni akimkabidhi tuzo maalum ya shirikisho hilo, Kocha mstaafu wa timu ya

taifa, Taifa Stars, Marcio Maximo

 

BABA na mamalishe wakiwa kazini katika Viwanja vya Maonyesho vya Mwalimu J. K Nyerere

 

RAIS Amani Abeid Karume wa Zanzibar, akisalimiana na Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki

 Thabo Mbeki

 

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),  Mama Salma Kikwete, akikata utepe...

Magazeti Yetu

Habari za Kitaifa, Kimataifa, Uchumi, Biashara na Michezo kila siku

Habari za Kitaifa, Kimataifa, Uchumi, Biashara na Michezo kila Jumapili

Habari za Michezo, Tamthilia, Makala na Burudani kila Alhamisi

Toa Maoni Yako

Hali ya Kisiasa Tanzania