Uhuru Publications Ltd - Gazeti Uhuru, Mzalendo na Burudani

Sunday
Sep 05th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size

Simulizi za Mastaa

E-mail Print PDF
Article Index
Simulizi za Mastaa
Messi awajaza matumaini wenzake
All Pages

Zidane: Kaka, Benzema watafanikiwa Madrid

MADRID, Hispania

MWANASOKA mkongwe Zinedine Zidane ‘Zizou’ amesema kuwa Kaka na Karim Benzema watapata mafanikio katika klabu ya Real Madrid licha ya kukosa mafanikio yaliyotarajiwa Bernabeu.

Kama Zidane, Kaka alitua katika klabu hiyo msimu huu akitokea AC Milan ya Italia na alitarajiwa angefanya mambo mengi makubwa, lakini ameshindwa kutoa mchango huo.

Karim Benzema, ambaye ni Mfaransa kama alivyo Zizou naye katika klabu hiyo amekuwa na kipindi kibaya na kizuri tangu asajiliwe na Real Madrid akitokea Lyon.

Zizou amesema wachezaji hao watatoa mchango mkubwa katika klabu hiyo baadaye na kamwe hawawezi kukwepa lawama kutoka kwa mashabiki kwani na yeye aliposajiliwa alikumbana nazo.

"Kama ilivyo kawaida hapa Madrid, kuna shutuma. Hivyo ndivyo ilivyo. Baada ya miezi miwili na mimi nilikutana na hali hiyo. Wote ni wachezaji wenye vipaji watafanikiwa," Zidane alisema.



Last Updated ( Thursday, 03 December 2009 11:22 )  

Magazeti Yetu

Habari za Kitaifa, Kimataifa, Uchumi, Biashara na Michezo kila siku

Habari za Kitaifa, Kimataifa, Uchumi, Biashara na Michezo kila Jumapili

Habari za Michezo, Tamthilia, Makala na Burudani kila Alhamisi

Toa Maoni Yako

Hali ya Kisiasa Tanzania